MAFUNZO YA NDOA

Kituo cha Usimamizi wa Masuala ya Familia cha Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro Kikishirikiana na taasisi ya An-Nahl Trust Kimeendesha Mafunzo ya Ndoa kwa siku mbili kwa Walioko na Wasioko kwenye Ndoa. Mafunzo hayo yalifanyika tarehe 1 hadi 2 Januari 2022. Mafunzo haya Yaliwashirikisha Washiriki Wapatao 25 Kutoka Maeneo Tofauti ya Dar es Salaam na Morogoro. Washiriki hawa Walijifunza Mambo Yafuatayo:

1-Misingi ya Ndoa katika Uislamu

2-Uchaguzi Sahihi wa Mwenza

3-Uchumi wa Familia na Athari zake katika Kuimarisha Ndoa

4-Mawasiliano kwa Wanandoa

5-Sababu za Migogoro na Utatuzi wake

6-Nyumba ya Muislamu

Mafunzo haya Yaliendeshwa na Wawezeshaji hawa Wafuatao:

Dkt. Bilal Juma

Iddi Jengo